Friday, February 14, 2014

Valentines Special

Huhitaji kuwa Mganga wala Mchawi kujua mambo haya yatatokea leo...

1.Pharmacy zitatengeneza hela nyingi sana kwa mauzo ya After Morning Pills baada ya watu kula rosti maini bila maji.Wauzaji wamenihakikishia mzigo upo wa kutosha,unaweza kukosa Panadol lakini sio Postinor2

2.Vyumba Vimejaa ndio habari ya mjini.Wahi booking mapema lasivyo utajikuta unaenda gesti Kibaha.Wamiliki wa Gesti wameniambia wameongeza Mataulo,Mashuka na Sabuni za EVA maana Short Time zitakuwa kibaooo.WANAWANGOJEA KWA HAMU wale wazee wa Mahali unapotoka....DAR.....Mahali unakoelekea....DAR

3.Sicksheet maofisini zitakuwa nyingi mabosi mjiandae.Wengine wamepanha kuugua tumbo kuanzia leo sa8 mchana.ili waseme wamekutwa na Typhoid hawaji kazini.Waandalieni MEMO

4.Mpenzi wako ataibiwa simu akiwa Mwenge stendi na hatapatikana siku yote eti ANARENEW LINE mpaka yapite masaa 24.UMELIWA Babe ake.

5.Utaombwa Dinner mapema sana sa12 au 1 usiku kwa kisingizio sa5 ameitwa home Mamake anaumwa kumbe ana Mchepuko,dinner ikiisha anakurudisha home anabadili nguo anaupitia mchepuko ambao umeahidiwa Romantic Dinner mida ya sa5 na watalala wote.We umerudishwa ukajikande ili mchepuko ukapewe Kabang.
USISEME SIKUKWAMBIA..

No comments:

Post a Comment