Sunday, January 18, 2015

INTERVIEW WITH DEBORAH / CANDY


MTB: MAMBO?
Deborah: Poa

MTB: POLE NA HONGERA KWA SHUGHULI ZA MAISHA.
Deborah: Asante sana. Namshukuru Mungu.

MTB: KWA FAIDA YA WASOMAJI, NAOMBA UTUAMBIE JINA LAKO KAMILI
Deborah: Jina langu la ubatizo naitwa Deborah Vicencia Myren Kerenge

MTB: JINA LAKO LA USANII JE?
Deborah: Najulikan kama Candy a.k.a Mama Msaliti
Deborah: Ila ukitaja tu Candy kila mtu anajua ni Nani.

MTB: HAHAHAHA...SAWA.
Deborah: (smiling)

MTB: MAJINA YAKO YA USANII UMEYAPATAJE?
Deborah: Jina la Candy lilianza kwenye group inayoitwa AFRICAN YOUTH ya Norway. Tulikua wadogo tukiingia studio kila mtu anajibatiza jina lake la kurap,na mimi nikaandikaga wimbo unaitwa they call me C.A.N.D.Y tangu siku hiyo nikaanza kuitwa Candy mpaka Leo kuna wasio Lijua jina langu la ubatizo.

Deborah: Mama Msaliti nilipewa na Christian Bella baada yakuwepo kwenye Video 
yake inayovuma sana nchini Tanzania (MSALITI).


MTB: SAWA.
MTB: NAOMBA UTUPE HISTORIA YAKO YA MAISHA KWA UFUPI, KAMA VILE UMEZALIWA WAPI MPAKA SASA UNAFANYA NINI.
Deborah: Bila shaka.
Deborah: Nimezaliwa miaka ya 80 Nakitu Musoma Tanzania,ni mtoto wa pili katika familia. Nina dada mkubwa na wadogo wanaonifuata.Nimeishi na kusoma Dar pamoja na Iringa Tosamagang.Nilivyofika miaka 13, kama sikosei, nikahamia Sweden /Norway. Kwa sasa ni Psychiatric nursing Assistant. Nabado ninaendelea kusoma Sweden.Vilevile mimi ni mwanamke ninaependa kujituma kwahiyo i'm a business Woman nauza vitu mbalimbali nakujishungulisha na mambo madogomadogo apart from my job.

MTB: HONGERA KWA KUWA MTU ANAYEJITUMA
Deborah: Shukran shukran.

MTB: SABABU KUBWA YA INTERVIEW HII NI TETESI NILIZOPATA KUWA UNAHAMA FANI, KUTOKA KUWA VIDEO VIXEN NA KUWA MSANII, JE NI ZA KWELI?
Deborah: Kwa furaha moyoni napenda nikwambie kua ni kweli kabisa.


MTB: UNAIMBA STYLE GANI YA MUZIKI?
Deborah: Mimi ni mpenzi wa Reggae Zouk na vilevile Old school HIP HOP. Kwa sasa wimbo ambao utatoka hivi karibuni ni wa HIPHOP umekaa kisexysexy flani siunajua tena swaga flani hivi amazing. Na mwingine ambao naufanyia kazi upo studio Jamaica ni Zouk imemix na reggae.

MTB: HAHAHAHAH, SAWA.
MTB: MPAKA SASA UMEANDAA NYIMBO NGAPI?
Deborah: Nimeandaa Nyimbo mbili mpaka sasa.Sema huwa ninarecord then naacha but sasa niko tayari na nina amini nimewiva, uwoga kwisha. So nawaahidi mambo mapya na mazuri katika muziki wakiafrica.

MTB: TUNAKUSUBIRI KWA HAMU
Deborah: Asante, very soon mtaniona.


MTB: JE UMESHIRIKISHA MSANII MWINGINE YEYOTE KWENYE HIZO NYIMBO MBILI ULIZOZIANDAA?
Deborah: Yes kwenye wimbo wa Hiphop unaotoka hivi karibuni nimemshirikisha mwanamziki aitwae Puzzo known as blackcurtains na ni Producer mzuri sana anayefanya kazi na wanamuziki wengi sana hapa Sweden.

MTB: LINI TUTEGEMEE VIDEO ZA KAZI ZAKO? NA JE UNAFANYA VIDEO SHOOTING SWEDEN?
Deborah: Nisingependa kutaja mwezi siku wala tarehe. Siunajua mambo mazuri yakiwa Suprise ndio fresh. Ila mjue ni anytime from now. Kuhusu video Ya Hiphop inafanyika huku huku Sweden, zifuatazo ninafanyia Jamaica na homeland Tanzania.

MTB: TUNAZISUBIRI KWA HAMU.
MTB: JE NI MSANII GANI WA TANZANIA UNGEPENDA KUFANYA NAE KAZI?
Deborah: Kwa HipHop ningependa kufanya kazi na Mwana F.A,Zouk ningependa kufanya na Alikiba na Christian Bella.
Deborah: Bila kusahau kuna wimbo wa bongo flava ambao ntafanya na BabyJ nishukapo Tz.



MTB: KUNA TETESI KUWA ULE WIMBO WA DULLY SYKES WA BABY CANDY AMEKUIMBA WEWE, JE KUNA UKWELI WOWOTE?
Deborah: Kiukweli Dully nimeshakutana nae na alisema wimbo kaniimbia mimi sasa nivigumu mimi kuingolea nafsi yake kama nikweli au sio.Ukweli anao yeye Dully (smiles).

MTB: HAHAHA, SAWA.
MTB: KWA VIDEO UTAZOFANYA TANZANIA, DIRECTOR GANI UNGEPENDA KUFANYA NAE KAZI?
Deborah: Kwasababu sijafika Tz muda mrefu sana nivigumu kusema ila so far namkubali Nisher, Adam Juma na Jerry Mushala.

MTB: UNA UJUMBE GANI KWA MASHABIKI WAKO?
Deborah: Wazidi kuniamini kama wanavyoniamini na wazidi kunipa moyo ili niendelee kufanya vizuri.Naahidi kuwaburudisha ipasavyo nasitowalet down

MTB: ASANTE SANA KWA INTERVIEW
Deborah: Nashurukuru pia.


MTB: TUNASUBIRI KAZI ZAKO KWA HAMU.
Deborah: Hivi karibuni mtafurahi.


No comments:

Post a Comment